Pages - Menu

Jumamosi, 8 Juni 2013

ALIETUHUMIWA KUMUUA BABA WA RAP QUEEN KUTOKA KENYA STELA MWANGI AHUKUMIWA



Mwezi wa kwanza mwaka jana, baba mzazi wa Rap Queen kutoka Kenya STL, Mr Jeff Mwangi Kwirikia, aliuwawa baada ya kugongwa na aliemgonga kukimbia katika manispaa ya Ullensaker huko Norway.

Ni zaidi ya mwaka sasa tangu ajali hiyo itokee, na mtuhumiwa huyo kajisalimisha mwenyewe wiki hii kwenye mamlaka husika, hatimae haki kupatikana kwa familia ya STL.

Kutokana na mtandao wa Norway, News In English, dereva huyo amehukumiwa kwa kumgonga kwa bahati mbaya na kumuua Mr. Mwangi katika ajali ya kugonga na kukimbia, na kuhumiwa kifungo cha siku 120 jela siku ya jumanne, lakini pia mahakama hiyo pia imemhukumu mwnaume huyo mwenye miaka 40, kutokuendesha gari tena maishani mwake na zaidi wakamuamuru kuwalipa member wa familia ya mzee Mwangi yenye watu 8 kiasi cha shilingi 35,393,250.00 kwa kila mmoja.

STL, ni mmoja kati ya wale waliofanya show ya uzinduzi wa BBA "The Chase" 2013, wengine ni pamoja nan Wande coal, Don Jazzy pamoja na D’Prince.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

HAPPY BRITHDAY TWALIB KIZIBO